Overblog
Editer l'article Suivre ce blog Administration + Créer mon blog

Mimi, Umma Party na Mapinduzi ya Zanzibar

🇹🇿 Hashil Seif Hashil alizaliwa kwenye ngarawa katika maji ya bahari ya Pemba Januari 12, 1938. Alisoma skuli ya msingi ya Mkwajuni na baadaye katika iliyokuwa Seyyid Khalifa Secondary Technical School, Beit-el-Ras, Unguja. Alikuwa ni mmoja wa vijana wafuasi wa Abdulrahman Babu waliopelekwa Cuba kwa mafunzo ya kijeshi kabla ya Mapinduzi ya Januari 12, 1964.  Baada ya Mapinduzi alipelekwa Indonesia kusomea sayansi ya ubaharia kwa miaka miwili na pia alipelekwa China kusomea uanamaji.Hashil Zanzibar alifanya kazi mbalimbali aliwahi kuwa afisa wa tatu katika meli za MV Africa na MV Jamhuri.  Alipouliwa Rais wa Zanzibar, Sheikh Abeid Amani Karume 1972, Hashil alikamatwa na kuwekwa jela ya Ukonga, Dar es Salaam, kwa muda wa miaka sita. Alipofunguliwa alikwenda Denmark kama mkimbizi. Baada ya miaka mitano akawa raia wa Denmark. Alifanya kazi katika meli mbalimbali za Kideni na baadaye alifanya kazi kwa miaka 20 katika Shirika la Haki za Binadamu la Denmark. Hashil ni mshairi na mwandishi wa vitabu vya riwaya.

🇫🇷 Mimi, Umma Party na Mapinduzi ya Zanzibar, en français, l'Umma Party, la révolution de Zanzibar et moi, est le livre de mémoires politiques d'Hashil Seif Hashil écrit en kiswahili. Hashil Seif Hashil est né sur une pirogue dans l'eau de l'océan indien à Pemba le 12 janvier 1938. Il fit partie des jeunes partisans d'Abdelrahman Babu qui furent envoyés à Cuba pour des enseignements militaires avant la révolution du 12 janvier 1964. Aprés la révolution il fut envoyé en Indonésie pour des études de sciences maritimes de deux ans puis en Chine pour apprendre la navigation. Il obtint de retour à Zanzibar le grade de lieutenant dans l'armée de marine puis il fut promu au grade de capitaine sur un navire de guerre. Après l'assassinat de Cheikh Abeid Amani Karume en 1972, Hashil Seif Hashil fut arrêté et incarcéré pendant six ans à la prison d'Ukonga à Dar -es-Salaam. Il fut admis comme réfugié au Danemark après sa libération. Il exerça ensuite diverses activités dans la marine marchande danoise puis fut pendant vingt ans un membre de la ligue des droits de l'Homme danoise. Hashil Seif Hashil est aussi un poète et l'auteur de romans.

Tag(s) : #Swahili Books, #Hashil Seif Hashil, #Zanzibar
Partager cet article
Pour être informé des derniers articles, inscrivez vous :